Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Frank - Walter Steinmeier amewaalika mawaziri wenzake kutoka Urusi, Ukraine na Ufaransa mjini Berlin siku ya Jumatatu kujadili utekelezaji wa makubaliano ya amani yaliyofikiwa mjini Minsk kuhusu mashariki mwa Ukraine, nchini Belarus Februari mwaka huu.
Mzozo kati ya waasi wanaoungwa mkono na Urusi na majeshi ya serikali ya Ukraine mashariki mwa nchi hiyo umesababisha watu 6,000 kupoteza maisha.
Viongozi wa Ujerumani na Ufaransa wamesimamia upatikanaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano mjini Minsk katika juhudi za kusitisha umwagikaji wa damu , na uhasama umepungua licha ya kuwa tofauti bado zipo katika kupiga hatua.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa Laurent Fabius anaamini kwamba hatua kiasi za maendeleo zimefikiwa ndani ya eneo hilo la vita licha ya ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano.
Tukio hilo lililochukua muda wa masaa 16 lilimalizika wakati washambuliaji wanne wameuwawa ama kujiripua. Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa katika shambulio hilo. Wizara ya elimu imekana ripoti kuwa wanafunzi 166 bado hawajulikani waliko.